Vyama vya Vijana – 1

UTUME KWA VIJANA 6
Sahaya G. Selvam, SDB

Vyama Mbalimbali na Malezi ya Vijana
 
Kuwapenda watu, na kupendwa na watu ni mojawapo ya mahitaji ya kila binadamu. Hitaji hili linaamshwa wakati wa ujana. Hali hii hutokana na mabadiliko ya kimaumbile, kihisia na ya kiakili yanayotokea wakati wa ujana.  Ndiyo maana vijana huwa wanahangaika sana na suala la kutafuta marafiki na namna ya kukuza mahusiano na watu, hasa uhusiano na watu wa jinsia tofauti.
 
Malezi ya jumla kwa vijana yanapaswa kuwapa vijana nafasi ya kukomaa kihisia na kijamii. Ukomavu huu unaweza kukamilishwa kwa njia ya vikundi na vyama vya vijana. Hakuna anayeweza kujifunza namna ya kujenga mahusiano yanayofaa isipokuwa kwa njia ya kupata nafasi ya kuwa katika mazingira ya kuzoeana na watu.  Kazi ya vyama vya vijana ni kuwatengenezea vijana mazingira haya.  Vijana wenyewe wanapenda sana kujiunga na vikundi mbalimbali na kushiriki katika shughuli za vikundi kwa sababu ya hitaji lao la kupenda na […]

Continue reading


Vyama vya Vijana -2

UTUME KWA VIJANA 7
Sahaya G. Selvam, SDB

Mambo Yatiayo Chachu katika Vyama vya Vijana

 
Katika makala iliyopita nilieleza kuhusu umuhimu wa vyama katika malezi ya vijana, niliorodhesha pia aina za vyama pamoja aina mbalimbali za shughuli zinazoweza kufanyika katika vikundi vya vijana.  Katika makala hii ningependa kutaja na kueleza vipengele vichache vinavyosaidia kufanikisha vyama vya vijana.
 
 
1. Mfumo na Uongozi
 
Endapo chama cha vijana kitafanikiwa kutolea malezi ya jumla kwa vijana ni lazima kiwe mfumo mzuri, pamoja na uongozi bora. Ingawa mfumo wa chama unaweza kuwa tofauti kadiri ya malengo yake, hapa tunaweza kutaja mfumo wa jumla ambao unafaa kwa chama chochote kile.  Kila chama kina wanachama wake, na viongozi wake ambao wanachaguliwa au kuteuliwa na wanachama. Uongozi unaweza kuundwa na watu kama watatu au watano kadiri ya mahitaji ya chama. Kuwa na watu wengi katika uongozi hakusaidii sana.   Aidha, kila chama cha vijana lazima kiwe na mlezi, walau mmoja,  […]

Continue reading