Lectio Divina

UTUME KWA VIJANA 12
Sahaya G. Selvam, SDB
 
Lectio Divina Kwa Vijana
 
Tangu mwaka 1985, imekuwa desturi katika Kanisa Katoliki kuadhimisha Jumapili ya Matawi kuwa Siku ya Vijana Duniani. Aidha, kila mwaka katika adhimisho hili Baba Mtakatifu huwa anatoa ujumbe maalumu kwa ajili ya vijana duniani kote.  Hata mwaka huu wa 2006, katika adhimisho la 21 la Siku ya Vijana Duniani (9 April 2006), Baba Mtakatifu ametoa ujumbe kwa vijana wote: “Dhamira ninayopendekeza kwenu ni kutoka Zaburi 119: 105 –  “Neno lako ni taa ya kuniongoza, na mwanga katika njia yangu.”
 
Katika ujumbe wake anasisitizia kuwa vijana wa siku hizi tunaishi katika mazingira magumu yenye falsafa za uongo na maadili potofu.  Katika mazingira haya ya giza Neno la Mungu ndilo linaloweza kuiangaza njia yetu.
 
Papa anatukumbushia maneno ya mwandishi wa Waraka kwa Waebrania anayesema: “Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo […]

Continue reading