Vyama vya Vijana -2

UTUME KWA VIJANA 7
Sahaya G. Selvam, SDB

Mambo Yatiayo Chachu katika Vyama vya Vijana

 
Katika makala iliyopita nilieleza kuhusu umuhimu wa vyama katika malezi ya vijana, niliorodhesha pia aina za vyama pamoja aina mbalimbali za shughuli zinazoweza kufanyika katika vikundi vya vijana.  Katika makala hii ningependa kutaja na kueleza vipengele vichache vinavyosaidia kufanikisha vyama vya vijana.
 
 
1. Mfumo na Uongozi
 
Endapo chama cha vijana kitafanikiwa kutolea malezi ya jumla kwa vijana ni lazima kiwe mfumo mzuri, pamoja na uongozi bora. Ingawa mfumo wa chama unaweza kuwa tofauti kadiri ya malengo yake, hapa tunaweza kutaja mfumo wa jumla ambao unafaa kwa chama chochote kile.  Kila chama kina wanachama wake, na viongozi wake ambao wanachaguliwa au kuteuliwa na wanachama. Uongozi unaweza kuundwa na watu kama watatu au watano kadiri ya mahitaji ya chama. Kuwa na watu wengi katika uongozi hakusaidii sana.   Aidha, kila chama cha vijana lazima kiwe na mlezi, walau mmoja,  […]

Continue reading


Vijana na Vyombo vya Mawasiliano

UTUME KWA VIJANA 8
Sahaya G. Selvam, SDB
Vijana na Vyombo vya Mawasiliano

Tupende tusipende nyakati hizi za karne ya 21 tumelazimika kutumia vyombo mbalimbali vya mawasiliano, kama vile, magazeti, simu, redio, kinasa sauti, runinga, video, mtandao, n.k. Vyombo hivi vimechangia katika kufanyia dunia yetu kuwa ndogo sana.  Vinachangia katika kuendeleza utandawazi, na katika usambazaji wa utamaduni wa kimagharibi.  Tunaweza kuvitumia vyombo hivi kwa ajili ya kujielimisha na kujiburudisha.  Maendeleo ya vyombo hivi yanatubabaisha.  Yaani, kila wakati vyombo hivi vinakuwa vya teknolojia mpya na vya rahisi kutumia.
 
Kwa vile, ni kawaida kwa vijana kuvutiwa na mambo mapya, hata maendeleo ya vyombo vya mawasiliano yanawashangaza sana. Vijana wanapenda pia kuunganika daima na vijana wenzao kwa njia ya kuvitumia vyombo hivi.  Kwa hiyo, wao huwa wanapenda kuzitumia aina mpya za vyombo vya mawasiliano, na pia kuvitumia sana.
 
Dunia ya mawasiliano inaweza kuchochea ubunifu wa vijana. Inaweza kuwasaidia kujielimisha na kujiburudisha. Aidha, inaweza kusababisha vijana kupoteza mali na […]

Continue reading


Siku ya Vijana Duniani

UTUME KWA VIJANA 9
Sahaya G. Selvam, SDB
 
“Tumekuja Kumwabudu”
Siku ya Vijana Duniani na Utume Kwa Vijana
 
Tarehe 16 hadi 21, mwezi Agosti, mwaka 2005 vijana wapatao millioni moja wanatarajiwa kukutanika huko Koloni nchini Ujerumani.  Kongamano hili limekuwa maarufu sana na linajulikana kwa jina la “Siku ya Vijana Duniani” – World Youth Day.  Siku ya Vijana Duniani (SVD) huadhimishwa kila mwaka katika majimbo ya Kanisa Katoliki siku ya Jumapili ya Matawi.   Lakini mara kwa mara huadhimishwa kimataifa, kwa muda wa wiki moja, kama hii ya mwaka huu huko Koloni. Kwa kawaida, kabla ya wiki ya kongamano lenyewe vijana hukaribishwa katika majimbo mbalimbali ya nchi husika. Wiki kabla ya SVD katika majimbo inawapa vijana wageni nafasi ya kushiriki katika maisha ya vijana wenyeji, na kubadilishana mawazo kuhusu matatizo ya dunia na hali ya Kanisa.  Wiki ya “World Youth Day” yenyewe ina vipindi vya Katekesi, nafasi za sala, na hija; wiki ya kongamano hufungwa kwa […]

Continue reading


Maisha ya Kiroho – 1

UTUME KWA VIJANA 10
Sahaya G. Selvam, SDB
 
Vijana, Tunaitwa kuwa Watakatifu!
Maisha ya Kiroho Kwa Vijana – 1
 
Sote Tumeitwa kuwa Watakatifu
 
Mtaguso wa pili wa Vatikano ulitukumbusha kuwa sisi sote tumeitwa kuwa watakatifu:  “Bwana Yesu, aliye Mwalimu na mfano wa kimungu wa kila ukamilifu, aliwahubiria wafuasi wake, wote na kila mmoja wa kila cheo na hali, utakatifu wa maisha, ambao Yeye huwa mtungaji na mtimilizaji wake. ‘Muwe wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu’ (Mt. 5:48).” (Hati ya Mwanga wa Mataifa, na. 40)
 
Kila mmoja katika maisha yake ya kila siku, anatafsiri agizo hili la Yesu kadiri ya nafasi yake na tena kulingana na wito wake – kama mlei, mtawa au padre.   Ingawa kila mmoja anaishi maisha yake kwa namna tofauti, wito wa kuwa mtakatifu ni mmoja.  Katika miaka iliyofuata Mtaguso wa pili wa Vatikano kanisa limeonesha wazi kwamba kuwa utakatifu si jambo la zamani, wala si nafasi pekee kwa wamonaki tu.  Kudhihirisha […]

Continue reading


Maisha ya Kiroho – 2

UTUME KWA VIJANA 11
Sahaya G. Selvam, SDB
Vijana, Tunaitwa kuwa Watakatifu!
Maisha ya Kiroho Kwa Vijana – 2
 
Katika makala iliyotangulia tulieleza kuhusu maana ya maisha ya kiroho kwa vijana.  Hapo chini tungependa kueleza vipengele saba vinavyoweza kuwasaidia vijana katika safari yao ya kujikamilisha.  Katika kuandika makala hii nimesaidiwa na Prosper Dionis, ambaye ni kijana mtanzania.  Kwa namna nyingine anaeleza jinsi yeye mwenyewe anavyoishi maisha ya utakatifu.
 
1. Kuadhimisha Maisha kwa Furaha
 
Kuadhimisha maisha kwa furaha ni ile hali ya kutambua ubora wa maisha na kutoruhusu mahangaiko ya maisha kutukatisha tamaa.  Maisha ni zawadi ya pekee kutoka kwa Mungu.  Zawadi hii ni kwa ajili ya kulindwa, kukuzwa na kuadhimishwa.  Taabu za maisha wala mahangaiko ya kila siku hayapaswi kuwa vizuizi vya sisi kutofurahia maisha. Kuadhimisha maisha kwa furaha ni fikra niliyo nayo kwamba maisha ni zaidi ya magumu ninayokutana nayo kwa sasa.  Kuadhimisha maisha ni kupokea zawadi ya maisha kama yalivyo, pamoja na taabu na […]

Continue reading